Makahaba mapacha wakongwe zaidi, Amsterdam.


Makahaba mapacha Louise na Martine
 
Makahaba hawa wameangaziwa kufuatia kutolewa kwa kumbukumbu zao na Filamu inayohusu maisha yao. Filamu hiyo, (Meet the Fokkens), inawaangazia Makahaba mapacha wenye umri wa miaka 70 Louise na Martine Fokken ambao walitufichulia siri yao katika kufanya ukahaba katika Mji maarufu zaidi kwa ufuska duniani.
Louise na Martine hutumia muda wao mwingi wakiwa kwenye Maskani yao ya vyumba viwili katika eneo la Ijmuiden,


Martine bado anafanya Ukahaba. Anasema malipo ay uzeeni anayopata kutoka kwa Serikali ya Uholanzi hayamtoshelezi kujikimu kimaishai. Isitoshe anaugua ugonjwa wa Baridi yabisi.
Martine anasema ijapokuwa angependa kustaafu lakini hawezi kuendelea kujikimu kimaisha. Filamu inayomuhusu inamuonyesha akiwa kazini, amejipachika kwenye kiti akiwa amevalia soksi ndefu, mshipi na viatu vya kisigino.

Martine Fokken ni kivutio kwa wanaume wakongwe badala ya vijana wanaompita bila hata kumtazama na kumkejeli kuwa amezeeka mno. Kama kawaida yake, anaangua kicheko na kusema hajali kamwe.
Anasema nyakati zimebadilika: "Vijana wa sasa ni tofauti, wanakunywa pombe sana, wamenona na hawakuheshimu. Wanapaswa kuwa kwenye pikipiki zao kama wavulana wa Kidachi badala ya kupoteza wakati wakinywa pombe."
Licha ya ushindani mkali kutoka kwa Vidosho wenye umri mdogo katika eneo la karibu, Martine hakosi wateja.
Anaonekana kuwavutia zaidi Wanaume wazee. Yeye hutumia vitu wanavyopendelea kuvaa ili kuwavutia kama vile kuingia kwenye madanguro akiwa na mjeledi huku amevaa viatu vya kisigino kirefu.

No comments:

Post a Comment