Ghafla isivyo tarajiwa, bilionea mmoja nchini Hong Kong amejitolea kumwaga dola milioni kwa 64 sawa na Paundi milioni 40 ambapo kwa hela zetu za madafu ni bilioni 120, na milioni 400 kwa mwanaume yeyote atakayejitokeza kumuoa binti yake mwenye tabia za kisagaji.
Tajiri huyo mfanyabiashara yuko tayari kutoa mkwanja huo wa hatari kwa mtu atakayemchukua binti huyo ila awe mwerevu, msomi na asiwe ni kwa nia za kujitafutia kipato.
Papaa huyo wa China Cecil Chao Sze-tsung amefikia hatua hiyo kufuatia taarifa kumfikia kuwa binti yake huyo Chao ana mahusiano ya kimapenzi na Sean Yeung  uliodumu kwa muda wa miaka saba (7) nchini Ufaransa.
Binti huyo Chao ambaye ni Mhitimu wa Chuo Kikuu cha Manchester na pia Mkurugenzi wa Makampuni na Biashara za Baba yake, Anaendesha Kampuni ya walimbwende ya Monde Talent na pia Afisa Uhusiano wa kampuni kubwa nchini Hong Kong.
Hata hivyo Bilionea Cecil Chao amesema hamlazimishi binti yake kuolewa ila atakayejitokeza atakula bingo.

Sean Yeung akiwa na mpenzi wake.
Baba na Mwana.