Diamond atoa tamko juu ya habari iliyoandikwa gazetini kuwa ana mahusiano mapya ya kimapenzi na binti kutoka Kenya


Majina ya Diamond na Wema yameshakuwa kama wimbo wa taifa katika magazeti maarufu kama ya udaku hapa Tanzania. 

Ikiwa ni wiki moja tu tangu Diamond afanye show huko Malindi nchini Kenya, gazeti la Risasi katika front page lilitoa story mpya inayomhusu Diamond, kuwa ana mahusiano mapya ya kimapenzi na binti kutoka Kenya na kichwa cha habari ni kama kinavyoonekana katika picha ya gazeti hilo hapo juu "WEMA, JOKATE MLIE TU!, DIAMOND ANASWA NA DEMU MPYAAA, Ni raia wa Kenya yadaiwa wana mipango mikubwa".

Diamond ameamua kuvunja ukimya kwa kutoa tamko lake kuhusiana na issue hiyo kupitia mtandao wake wa www.thisisdiamond.com. Na hiki ndicho alichokiandika:

"Dah! kiukweli nimesikitishwa sana na taarifa za mwanadada huyu kujinadi kua anamahusiano na mimi ya kimamapenzi na eti tunamipango mingi ikiwemo ya Harusi ndani yake...  dah! kiukweli nimejiskia vibaya sana Kwani taarifa azitoazo msichana huyo si za kweli kabisa, Nilikutana nae Malindi akiwa kama mmoja ya Waandaaji wa tamasha hilo niLIlokwenda kutumbuiza na mbali ya hayo pia alikua ni mdogo wa Mwenyeji wangu wa Malindi, hivyo nilikua nikimchukulia kama dada yangu kumbe mwenzangu alikua anamipango mingine...kiukweli nimejiskia vibaya, Nimehisi kama Ukarimu wangu kwake na kuwa nae huru kama mmoja ya wenyeji wangu umeniponza, badala yake anatumia picha tulizopiga nae kwa namana nyingine....Ukweli ni kwamba MWANADADA HUYO SINA MAHUSIANO NAE YA KIMAPENZI KABISA.... MPENZI WANGU NAAMINI KILA MTU ANAMJUA...."

No comments:

Post a Comment