Hiki ndicho Bonta angependa kitokee kwa makundi ya Hip Hop Tanzania, kuhusu alichosema Nikki Mbishi “No Comment”.


Bonta

Bonta a.k.a Maarifa hivi karibuni ameachia wimbo wake unaoenda kwa jina la ‘Tukutane Maktaba’ ambao umesababisha maoni mbali mbali kutoka kwa watu hasa kupitia mitandao ya kijamii kama facebook, wengi wakimpa big up kwa kazi yake, lakini pia alipata criticism toka kwa Nikki Mbishi wa Tamaduni Music ambae amekuwa akiandika status kuwamcriticise Bonta na baadhi Weusi.
Mweusi toka katika kundi la River Camp Soldiers alifanya interview na Josefly mtangazaji wa victoria fm iliyoko Musoma, kupitia kipindi cha Over drive.
The river camp doctor alifunguka mengi kuhusu ‘tukutane Maktaba’, kisha mtangazaji huyo aliuliza “baada ya kuachia ngoma yako watu wengi walionekana kuipokea vizuri kupitia mitandao mbali mbali ya kijamii na blogs mbalimbali, lakini kuna criticism, unamfahamu jamaa mmoja anaitwa Nikki Mbishi?” Bonta alijibu “ah, hiyo no comment, hilo siwezi  kuzungumzia kwa sababu kila mtu ana uhuru wa kuongea kitu chochote anachotaka kwenye nchi yetu, kwa hiyo no comment kwa hilo mtu wangu.”
Na kuhusu kile anachotamani kitokee kati ya makundi yote ya hip hop Tanzania ambacho kingemfanya aone kakundi yamepiga hatua Tanzania, alifunguka, “mi natamani kila kundi lifanye muziki wake na kila kundi litumie miguu yake kutembea kufika pale linapotamani na lisitumie mgongo wa kundi lingine, lisitumie midomo yao vibaya wala lisitumie freedom of speech vibaya, kila mtu afanye kazi yake na kila aheshimu kazi ya mtu, au sio, usitumie effort ya mtu ambayo ameshatengeneza ili upate negative publicity, at the  end of the day unajua mashabiki wako ndio mashabiki wangu, mashabiki wangu wataendelea kuwa mashabiki wangu na mashabiki wako wachache watakuja kwangu.”

No comments:

Post a Comment