Lord Eyez akirecord wimbo mpya...baadhi ya maneno "Too many fake people aah wamecheka aah naziona dimpoz..." Amzungumzia pia Ray C..



Producer P-funk Majani ametoa studio teaser ya Lord Eyez kwa njia ya video, ikimuonesha Mweusi huyo akiwa booth katika studio za Bongo Recordz... ikimaanisha alikuwa katika recording session ya wimbo unaoonekana kuwa ni mpya na unaozungumzia matukio ya hivi karibuni yaliyomhusisha Lord Eyez . 

Hii ni baadhi ya mistari inayosikika kwenye teaser hiyo:
“Mungu mmbariki Ray C mmbariki na mama yake, mtoe kwenye haya majanga mrudishie maisha yake....okay lete habari, Lord Eyez kafanya hivi na hivi uzeni hiyo habari, eeh mungu nibariki niepukane na hii hali, too many fake people, aaah wamecheka aaah naziona dimpoz, nini power windows Napata nikiuza....F***the power window big boy is innocent, naingizwa kwa majanga na sijala hata senti...........”

No comments:

Post a Comment