Justin Bieber azomewa na mashabiki wa mpira wa mguu nchini kwao Canada



Ule msemo wa nabii hakubaliki kwao umethibika kwa mwimbaji anaefunika katika majukwaa ya kimataifa Justin Bieber ambae alijikuta akizomewa wakati anajiandaa kupanda jukwaani kuimba wakati wa mapumziko katika mchezo wa mpira wa miguu huko nchini kwao.
Crowd ya Toronto ilianza kuzomea kwa nguvu baada tu ya kumuona Bieber kwenye screen kubwa ya uwanjani akiwa anasogea jukwaani kuimba hit songs zake mbili ‘Boyfrriend’ na ‘Beauty and Beat’.
Mashabiki hao walizomea tena pale ambapo jina la Bieber lilitajwa na MC uwanjani hapo. Bieber ambae ni mshindi wa American Awards kama msanii wa mwaka alionekana kutoteteleka na kuzomewa na akaendelea kupiga show hadi mwisho tena kwa nguvu ile ile.
Japokuwa watu walizomea tangu mwanzo hadi mwisho wa performance yake muda wote wakati timu ziko katika mapumziko, alimaliza nyimbo zote mbili bila kuonesha hisia yeyote mbaya kwa mashabiki, na Mcanada huyo alimalizia na sentensi mbili, “Thank you so much Canada. I love you.”
Mmoja kati ya football fans waliokuwa pale walielezea kwa nini watu walimzomea Biebs, “J-Biebs hashangilii mpira wa miguu, unajua, wala Carly Rae Jepsen pia,” alisema Ryan Prisque (22), shabiki toka pande za Calgary.
Ingawa Justin Bieber ni msanii mwenye umri mdogo anastahili kusifiwa kwa kuweza kuhimili changamoto kubwa kama hiyo na kuonesha anavyoiheshimu kazi yake na hisia za mashabiki wake iwe ni hisia positive ama negative, hilo ni moja kati ya vigezo vya ukomavu katika sanaa.

No comments:

Post a Comment