Angelina Jolie kung’atuka uigizaji ili awe mama wa nyumbani na alee watoto.


Angelina Jolie

Muigizaji wa kike Angelina Jolie aliyetamba sana na action movie ya Mr.&Mrs. Smith amefunguka katika interview aliyofanya na kituo cha televisheni cha Uingereza ‘4 News’ kwamba anampango wa kuachana na kazi yake ya uigizaji muda mfupi ujao.
Mshindi huyo wa tuzo za Oscar ambae yuko busy akiandaa movie yake ‘Maleficent’ anaona wakati umefika sasa anataka kuachia ngazi kwa sababu mbalimbali hasa sababu za kifamilia na majukumu ya kazi za nyumbani, “nadhani naelekea kuachana na uigizaji kwa wakati mwanangu anafikia umri wa miaka 13 hivi, anyway, shunguli nyingi sana za kufanya nyumbani.”

Angelina Jolie mwenye watoto sita alikiri kuenjoy kuwa muigizaji na ukizingatia yuko kwenye list ‘A’ ya Hollywood Stars, “nimekuwa naenjoy sana kuigiza, ninajivunia kuwa katika hii kazi na ninauzoefu mkubwa na nimekuwa na uwezo wa kusimulia hadithi na kuwa sehemu ya hadithi ambazo zinamaana na nimefanya mambo for fun, lakini...”, aliongeza ila hakumalizia sentensi yake na kutabasamu.
‘The Salt’ actress alielezea mipango yake kabla hajang’atuka katika tasnia hii ya uigizaji, “nitafanya movie kadhaa na nina bahati nzuri sana kuwa na kazi hii, ni taaluma yenye bahati ukiwa sehemu yake na ninaifurahia, lakini kama ntatoka kesho nitakuwa na furaha sana kuwa nyumbani na watoto wangu. Naamka asubuhi kama mama na ninaangalia habari kama mtu mwingine yeyote na naangalia nini kinatokea na nataka kuwa sehemu ya dunia katika njia chanya.” Alimaliza Angelina Jolie

No comments:

Post a Comment