NEWZ:Msaada kwa Rwanda wasitishwa.

 



Serikali ya Uholanzi imesitisha msaada wa dola milioni 6.15 kwa Rwanda baada ya nchi hiyo kuhusishwa na ufadhili wa waasi katika Jamuhuri ya kjidemokrasia ya Congo.
Hatua hii inajiri siku kadhaa baada ya Marekani kutangza inanuia kupunguza msaada wa kijeshi kwa Rwanda.

Hata hivyo Rwanda imekuwa ikikanusha madai ya umoja wa mataifa kuwa inafadhili kundi la waasi wa M23 mashariki mwa DR Congo.
Waasi hao walianza kutoka jeshini kuanzia mwezi Aprili na hadi kufikia sasa takriban watu 200,000 wametoroka makwao kwa sababu ya mapigano kati ya jeshi na waasi hao.

Hatua hii ya Udachi inajiri baada ya afisaa mkuu wa umoja wa mataifa kuambia BBC kuwa wanajeshi wanaotoka katika jeshi la DRC wamekiri kusajiliwa na Rwanda.
Mnamo siku ya Alhamisi, Umoja wa mataifa uliripoti kuwa wana
jeshi wake walisaidia jeshi la DRC kuwafukuza waasi hao kutoka mji wa Goma kwa kutumia helikopta pamoja na magari ya kijeshi.

No comments:

Post a Comment